KAMATI ya
wataalamu ya maswala ya habari Zanzibar
(ZAMECO) imekuwa mstari wa mbele katika harakati za kufuatilia mchakato wa
marekebisho ya sheria za habari ikiwemo sheria ya utangazaji No. 7 ya 1997
ambayo ilifanyiwa marekebisho na sheria No. 1 ya mwaka 2010.
Katika vikao mbali mbali
ZAMECO ilitoa mapendekezo kuhusu marekebisho ya sheria hio kwa lengo la
kupatikana kwa sheria mpya na rafiki kwa wandishi wa habari na vyombo vya
habari nchini.
Aidha, mnamo tarehe 9/4/2024
ZAMECO walifika katika Afisi za tume ya kurekebisha sheria Zanzibar iliyopo Vuga kwa ajili ya kufuatilia
hatua iliyofikiwa baada ya kupokea mapendekezo hayo mwezi wa Octoba mwaka 2023.
Mratibu wa baraza la habari
Tanzania (MCT) kwa upande wa Zanzibar Shifaa Said ameeleza kuwa, hatua hii ya
ufuatiliaji imechukuliwa ili kuhakikisha mchakato wa kupatikana kwa rasimu ya sheria
ya utangazaji unakwenda vizuri na
hatimae, sheria mpya itakayokidhi vigezo vya habari ipatikane.
Kwa upande wake, Salim Said
mwandishi wa habari mkongwe amesisitiza kwamba vyombo vya habari havina lengo
baya na Serikali, bali ni mdau wao muhimu katika kuleta maendeleo ya jamii,
hivyo jitihada za ZAMECO na wengine katika kuendeleza maboresho ya sheria ya
Utangazaji zinachukuliwa kama sehemu ya ushirikiano mzuri kati ya vyombo vya
habari na Serikali.
“ Vyombo vya habari havina
lengo baya na Serikali, kwani sisi ni washirika wazuri na wenye lengo jema kwa
jamii na Serikali kwa ujumla,kwa kuzingatia vyombo vya habari ni nguzo ya
maendeleo ya uchumi” alisema.
Katibu wa tume ya kurekebisha
sheria Zanzibar, Mussa kombo Bakar
aliwapongeza ZAMECO kwa jitihada wanazozichukuwa katika kutafuta maendeleo ya
tasnia ya habari nchini na kubainisha kuwa mapendekezo waliyowasilisha
yamepokelewa na kufanyiwa kazi.
Nae, mkurugenzi wa Chama cha
wandishi wa habari WanawakeTanzania ,Zanzibar (TAMWA ZNZ) Dkt Mzuri Issa ametoa
shukrani kwa katibu na wafanyakazi wote wa Tume kwa ushirikiano wao katika
mchakato huu wa kupata sheria mpya, huku akisisitiza umuhimu wa ushirikiano wao
katika mchakato huu,kwa kuhakikisha upatikanaji wa sheria mpya kwa maslahi ya
Zanzibar na wazanzibari wote.
Ni miaka 20 sasa wadau
wa maswala ya habari Zanzibar, wamekuwa
wakipambania marekebisho ya sheria mbali
mbali za habari, ikiwemo sheria ya
usajili wa wakala wa habari, magazeti na vitabu No.5 ya mwaka 1988 iliyifanyiwa
marekebisho na sheria No.8 ya mwaka 1997 na sheria ya utangazaji No. 7 ya 1997 ambayo ilifanyiwa
marekebisho na sheria No 1 ya 2010, ambayo oktoba mwaka jana tume ya kurekebisha
sheria Zanzibzr ilipokea mapendekezo ya marekebisho ya sheria ya utangazaji kwa
lengo la kupata sheria huru iliyokuwa rafiki kwa tasnia ya habari na jamii kwa ujumla.
MWISHO
Post a Comment