MTUHUMIWA KESI YA MAUWAJI ASOTA RUMANDE.


 NA MARYAM NASSOR ,

MTUHUMIWA   wa kesi ya kuuwa kwa makusudi,inayosikilizwa mahakama kuu Tunguu Zanzibar, inayomkabili  kijana Omar Mahmoud Abdallah (36) mkaazi  wa Jang’ombe Unguja,ameendelea kusota rumande,baada ya upande wa mashtaka  kushindwa  kukamilisha  upelelezi wa shauri hilo kwa wakati.

 Mara baada ya kufika mahakamani hapo, mtuhumiwa huyo akitokea rumande, mwendesha mashtaka kutoka ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka Zanzibar Said Ali Said

Alimueleza, Jaji wa mahakama kuu Zanzibar kuwa, kesi iyo ipo kwa ajili ya kuanza kusikilizwa  maelezo ya awali lakini  bado upelelezi wa shauri hilo haujakamilika.

“Muheshimiwa jaji leo, kesi hii ipo kwa ajili ya kusikilizwa lakini bado hatujakamilisha  upelelezi wa kesi na mashahidi, hivyo tunaomba utupangie tarehe nyengine kwa ajili ya kusikilizwa’’ alidai dpp huyo.

 Baada ya maelezo hayo, Jaji wa mahakama kuu Zanzibar  Ali Mohamed Ali  aliwauliza mawakili wa upande wa utetezi uliokuwa ukiongozwa na mawakili  wasomi  Ali Rashid Ali na Elia  Elisha  kuwa wanakubaliana na ombi la upande wa  mashtaka.

 Wakili wasomi, walidai kuwa hawana pingamizi  yoyote juu ya ombi hilo, ila wanataka upande wa mashtaka  kujihimu kukamilisha maelezo ya kesi na mashahidi illi kesi hiyo ianze kusikilizwa.

“ Hatuna pingamizi na upande wa mashtaka ila tunataka, wajihimu kukamilisha  maelezo ya kesi, ili mteja wetu ajuwe hatma yake mapema” walidai .

Jaji wa mahakama hiyo, aliuliza  upande wa mashtaka kuwa ni lini,  watakuwa wameshakamilisha maelezo ya kesi na mashahidi na kujibu hivi karibuni.

Jaji huyo, aliutaka upande wa mashtaka kuwa wanatakiwa kukamilisha  maelezo ya kesi na mashahidi kwa wakati ili kesi hiyo ianze kusikilizwa.

Kwa mara ya kwanza shauri hilo, lilisomwa mahakamani hapo  August 29  mwaka 2023 na kuhairishwa miezi mitatu  mfululizo,kutokana na kutokamilika kwa upelelezi wa kesi hiyo.

Awali ilidaiwa mahakamani hapo  na mwendesha mashtaka kutoka afisi ya mkurugenzi wa mashtka Zanzibar, kuwa mstakiwa huyo  anadaiwa kumuua kwa makusudi kijana Seif Omar Salum.

Mshtakiwa huyo, alitenda kosa hilo, huko Jang’ombe wilaya ya mjini, mkoa wa mjini magharibi  unguja majira ya saa 1:00  usiku.

Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa, kutenda  hivyo ni kosa kinyume na kifungu  cha 179 na 180 chini ya  kifungu namba 6 cha mwaka 2018  sheria za Zanzibar.

Jaji huyo, aliutaka upande wa mashtaka kukamilisha  upelelezi wa shauri  hilo, ili  kesi hiyo ianze kusikilizwa mahakamani hapo na kuihairisha kesi hiyo hadi machi 20 mwaka huu, kwa ajili ya kusikilizwa maelezo ya awali na mtuhumiwa kurejesha rumande.

No comments

Powered by Blogger.