KUELEKEA siku ya wanawake Duniani


 NA MARYAM NASSOR

KUELEKEA siku ya wanawake Duniani, Uongozi wa  serikali  ya wanafunzi chuo cha utawala wa umma Zanzibar Ipa,  kimeadhimisha  siku hiyo, kwa kupanda miti  katika skuli ya sekondari Jumbi  na Tunguu wilaya ya magharibi B  unguja, huku ikiwataka  wanafunzi wa skuli hizo  kuitunza miti hiyo.

Akizungumza na wanafunzi wa kike katika  skuli hizo kwa nyakati tofauti Rais wa serikali ya wanafunzi  chuo cha ipa, Nagila Abdalllah Ali  alisema lengo la ziara hiyo, ni kuja kuwapa wanafunzi hao  elimu ya mazingira, udhalilishaji na maswali ya uongozi ili waje kuwa viongozi bora wa baadae.

  Aidha, aliwata wanafunzi wa  kike kusoma kwa bidii na kufikia ndoto zao  za kielimu ili waje kuwa viongozi bora  wa baadae ndani ya familia  zao na taifa kwa ujumla.

Alisema kuwa, wanawake ni kundi kubwa katika jamii hivyo, wana dhima kubwa ya kuelimika na kuielimisha jamii juu ya   maswala ya udhalilishaji na matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii.

“Tumekuja hapa kwa lengo la kuwapa elimu  ya mazingira na  maswala  mazima ya udhalilishaji  na uongozi , ili  muje kuwa viongozi wazuri wa baadae ‘’ alisema.



Nae, Afisa sheria  wa wanawake kutoka ( zafela) Fatma Ali  Bakari aliwataka  wanafunzi wa kike  kusoma kwa bidii na kujikinga na mimba za utotoni  ili kufikia ndoto zao  za  kielimu.

Alisema kuwa,ni wajibu kwa kila mwanafunzi kusimamia masomo yake sambamba na kuacha tabia hatarishi  ambazo zitaweza kumharibia malengo yake.

‘’ Munatakiwa kusoma kwa bidii  na kuviepuka vishawishi  ili kuepukana na ndoa za mapema na kufikia malengo yenu ya kielimi ili muje kuwa viongozi bora wa baadae” alisema.

  Hivyo, aliwasisitiza wanafunzi hao kusoma kwa bidii na kuweza kujikinga na mimba za utotoni na kuacha tabia hatarishi.

Nae, mwenyekiti wa jumuiya ya vijana  wenye taaluma Zanzibar Nadia Mwinyi Aboud aliwataka wanafunzi hao kuweza kujiongoza  na kusimamia malengo yao ya kielimu.

Aidha aliwataka wanafunzi wakike kujua thamani zao kama wanawake ili wajuwe haki  na fursa  ambazo  zimewazunguka ili waweze kunufaika nazo.

Nae, mwalim wa mazingira na ustawi wa jamii katika skuli ya Jumbi, Nassor Haji Juma aliwashukuru viongozi wa serikali ya wanafunzi chuo cha ipa na ugeni  waliofuatana nao, na  kuwataka isiwe mwisho  waendelee kwenda kuwapa elimu.

Ziara  hiyo ya siku moja ya kupanda miti na kutowa elimu kwa wanafunzi wa kike, kuelekea  maadhimisho ya siku ya wanawake duniani  inayoadhimishwa  mach 8 ya kila mwaka yameandaliwa na uongozi wa ipa, wanasheria kutoka zafela na wasaidizi wa sheria Zanzibar.

No comments

Powered by Blogger.