MAJAJI WAANZA KAZI RASMI KUCHAMBUA KAZI ZA TUNZO YA UANDISHI WA HABARI ZA TABIACHI ZA '' COMMUNITY FOREST''


NA MWANDISHI  WETU,

JOPO la majaji limeanza rasmi kupitia na kuchambua kazi zilizowasilishwa na waandishi wa Habari na vyombo vya habari katika Tuzo ya Uandishi wa Habari za Tabianchi za Community Forests.

Mchakato huu ,ni hatua muhimu kuelekea hafla ya utoaji wa tuzo itakayofanyika tarehe 28 Machi 2026.

Kupitia tuzo hizo , Meneja wa Mawasiliano kutoka Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania Zanzibar  (TAMWA ZNZ ) Bi Sophia  Ngalapy  amesema  Community Forests Pemba, Community Forests International na TAMWA-ZNZ wanalenga kutambua na kuhamasisha uandishi wa habari unaoangazia mchango na uongozi wa wanawake katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi Zanzibar.

 Amesema Majaji hao, wanapitia kazi mbalimbali zilizowasilishwa kutoka vyombo tofauti vya habari ili kuhakikisha kuwa kazi zenye ubora na zinazobeba simulizi za mabadiliko chanya zinapata nafasi ya kutambuliwa katika tuzo hizo.

Jumla ya kazi 73 zimewasilishwa na waandishi wa habari kutoka katika makundi ya magazeti, redio, televisheni na mitandao ya kijamii, huku vyombo vya habari 7 kutoka Zanzibar.

 

No comments

Powered by Blogger.