WAANDISHI WA HABARI WAMETAKIWA KUHAMASISHA JAMII KURIPOTI VITENDO VYA RUSHWA KIPINDI CHA UCHAGUZI.
NA MARYAM NASSOR
MAMLAKA ya
kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar (ZAECA) imewataka wanawake wanaogombea
nafasi mbali mbali za uongozi kutoa
taarifa mapema za vitendo vya rushwa kwani kuna sheria inayomlinda shahidi na
mtoa taarifa.
Akizungumza katika mafunzo ya siku moja kwa
waandishi wa Habari Afisa Elimu na kinga
kutoka ZAECA, Yussuf Juma
huko katika Afisi za Chama cha Waandishi wa Habari
Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA ZNZ)
Tunguu Unguja.
Amesema, sheria ya ZAECA namba 5 ya mwaka 1992,
kifungu cha 98 kinamlinda mtoa taarifa na kifungu cha 99 kinamlinda
shahidi, hivyo ikiwa shahidi utapata ulinzi lakini pia ukiwa mtoa taarifa sheria inakulinda.
Amesema kuwa , Rushwa ndio kikwazo kikubwa kwa maendeleo ya kiuchumi, kijamii na kisiasa , hivyo ni vizuri jamii kushirikiana na mamlaka hiyo kwa kutoa taarifa mapema kabla tukio halijafanyika.
Aidha amesema
kuwa, silaha imara dhidi ya rushwa ni kila mtu kujitambua na kujua thamani yake kwa kufuata sheria na kutokuwa
tegemezi
“ Kesi
nyingi tunazozipata huwa zimeshatokea
aidha mtu kaahidiwa ajira kakubali kutoa
rushwa hatowi taarifa mpaka atakapokosa hiyo ajira ndipo anakuja kwetu katika
hatua za mwisho kabisa” amesema Yussuf.
Amesema kuwa,
vitendo vya rushwa kwenye uchaguzi vinatokea lakini taarifa hazifiki
kwao “rushwa ya ngono ipo lakini haizungumzwi kwa sababu watu wanaichukulia
kama Jambo la kawaida “ amesema .
Aidha
amewataka viongozi wanaogombea nafasi
mbali mbali za uongozi kufuata sheria na taratibu za nchi na za uchaguzi ili
wasiwe wao ndio visababishi vya rushwa.
“ Sababu kubwa za kutokea kwa rushwa ni
kuvunja sheria na taratibu na kanuni, kwani mtu ili agombee lazima awe na sifa za kugombea “ amasema.
Nae,
Mwezeshaji wa mafunzo hayo Asha Abdi Makame amewataka waandishi wa Habari
kuandika habari za mafanikioz za wanawake viongozi waliofanikiwa kuleta maendeleo.
Amesema
kuwa, kazi kubwa ya waandishi wa Habari ni kuibua na kutetea haki za wanawake,
hivyo ni vizuri kuelimisha jamii
kuhusiana na umuhimu wa wanawake kugombea nafasi za uongozi.
“ Jamii bado
haina uwelewa wa kutosha kuhusu umuhimu
wa wanawake kuwa viongozi, hivyo ni vyema waandishi wa habari kuandika Makala
na Habari za wanawake waliofanya vizuri kwenye uongozi ili waonekanae “
ameshauri .
Nao baadhi ya waandishi walioshiriki mafunzo
hayo, Maryam Naasor amewashauri
waandishi wachanga waliopata mafunzo
hayo, kujitoa zaidi ili kufanikiwa
katika kazi zao.
Amewataka waandishi hao , kushirikiana na waandishi wengine ambao wazoefu wapo katika mradi huo ili kupata urahisi wa kazi zao.
Awali mafunzo hayo, yalifunguliwa na Afisa program
wa mafunzo hayo ya waandishi wa Habari
wachanga (Young Media Fellows) Tatu Ali
ambapo aliwataka waandishi wa mradi huo kuendelea kuandika Habari za wanawake
na uongozi hasa kipindi kinachoelekea cha uchaguzi.
Mafunzo hayo ya siku moja , yamewashirikisha waandishi wa Habari 14 wa unguja kutoka
vyombo mbali mbali vya Habari nchini ikiwa ni muendelezo wa mradi wa YMF kutoka
TAMWA ZNZ.





Post a Comment