WANAWAKE TOENI TAARIFA MAPEMA ZA UDHALILISHAJI KABLA HAMUJAFANYIWA -TAMWA ZNZ.
NA MARYAM NASSOR
WANAWAKE
wanaotaka kugombea nafasi mbali mbali za
uongozi katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu, wametakiwa
kuripoti matukio ya
udhalilishaji katika hatua ya awali kabla
matukio hayo hayaja tokea.
Akizungumza katika kikao kazi cha kujadili viashiria vya udhalilishaji
kwa wanawake kipindi cha uchaguzi
na kampeni Afisa Tathmini na Ufuatiliaji
kutoka Chama cha wandishi wa Habari wanawake Tanzania Zanzibar ( TAMWA ZNZ)
Mohamed Khatib huko katika Ofisi ya
Chama hicho Tunguu Unguja.
Amesema , kipindi cha uchaguzi na kampeni
wanawake wanaogombea wamekuwa
wakikabiliwa na udhalilishaji mbali mbali ukiwemo udhalilishaji wa kimwili ,kingono na kisaikolojia.
Amesema kuwa
, TAMWA ZNZ ,kwa kushirikiana na Taasisi
ya demokrasia ya ( NDI) mwaka 2024 wamefanya utafiti na kugundua kuwa wanawake wanakabiliwa na udhalilishaji mkubwa katika kugombea nafasi mbali mbali za uongozi wa
kisiasa.
Aidha amesema kuwa, utafiti huo, umeonesha
kuwa wanawake asilimia 45 wanakumbana na udhalilishaji wa
kisaikolojia , asilimia 25 wanapata udhalilishaji wa kimwili na asilimia 22 wanakumbwa na udhalilishaji wa kingono.
“ Hivyo mwaka huu tunataka wagombea wanawake waripoti matukio hayo ya udhalilishaji wanayofanyia katika uchaguzi kabla ya kufanyiwa ili kujikinga na vitendo hivyo viovu “ amesema Mohamed.
Nae,
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake wenye
Ulemavu Zanzibar Salma Saadat amesema,
wanafanya ufuatiliaji wa matukio
hayo ili kuhakikisha mwaka huu hayajitokezi au yanapungua.
Amesema kuwa, lengo la kikao hicho na
kuwakutanisha viongozi mbali mbali
wa vyama vya siasa na kuwapa uwelewa wa kuweza kuripoti matukio hayo
pindi yakiwakuta.
“ Tunatamani
sana mwaka huu matukio ya udhalilishaji kwa
wanawake wanaogombea yasitokee lakini pia
yakiwakuta wawe tayari kuyaripoti ili
yaweze kuchukuliwa hatua” amesema bi Salma.
Nae Afisa kutoka Mamlaka ya kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar (ZAECA) Mgeni Salami amesema kuwa Serikali imeshaweka miongozo na sheria namba 5 ya mwaka 2023 ambayo inamlinda mtoa taarifa .
Amesema kuwa, sheria hiyo ya ZAECA adhabu yake ni kubwa kwani inaenda
sambamba mtuhumiwa atafungwa na atalipa
faini.
Hivyo, aliwataka wanawake ambao wanataka
kugombea katika uchaguzi wa mwaka huu 2025 kuwa na
uthubutu kwani kuna sheria inawalinda na
mtoa taarifa analindwa pia.
Omar
Hassan ni mkaguzi wa Jeshi la Polisi na
Afisa Habari wa Jeshi hilo amesema , wamejipanga katika uchaguzi huu
kuwalinda rai ana mali zao na yoyote atakayepata dhalilishwa kipindi cha uchaguzi atoe taarifa
na wao wataifanyiakazi.
Nae, Hasina Ali Mattar kutoka chama cha Wananchi ( CUF)
amesema ni kweli wanawake wanakumbana na vitendo mbali mbali vya
udhalilishaji kipindi cha kampeni na uchaguzi na kuahidi kutoa taarifa endapo
atafanyiwa vitendo hivyo.
Khadija Saum
Ali ni Katibu wa Kamati Maalum ya Maadili ya NEC kutoka Chama cha
Mapinduzi , amesema kikao hicho
kimewasaidia kujipanga kuelekea katika
uchaguzi mkuu kwani wanawake wana haki kisheria ya kugombea bila ya
kudhalilishwa.
Kikao hicho cha siku moja kimeandaliwa na
TAMWA ZNZ, Jumuiya ya Wanawake wenye Ulemavu Zanzibar JUWAUZA, Chama cha Wanasheria wanawake
Zanzibar ZAFELA na PEGAO kimewashirikisha
viongozi wa vyama vya siasa,
maafisa kutoka Jeshi la Polisi, Zaeca na Wandishi wa Habari.
MWISHO


Post a Comment