FAKIHAT MWANAMKE MWENYE NDOTO YA KUWA KIONGOZI KUWASAIDIA WATU WENYE ULEMAVU ZANZIBAR
Fakihat
– “Ulemavu huujazima sauti yangu ya kuwa kiongozi kwa jamii”.
Na
- Maryam Nassor.
Zanzibar:
‘’Naumia
nikiona watoto wenye ulemavu, hawapewi kipaumbele katika jamii kwani nao, wana haki
sawa ya kupewa elimu na kushirikishwa katika
kugombea nafasi za uongozi’’ Anasema Fakihat.
Fakihat Omar Abubakar,
23 ni miongoni mwa watoto wa kike,mwenye ulemavu, ambae ana ndoto kubwa ya kuwa
kiongozi ili kuisaidia jamii yake lakini pia, kuwasaidia watu wenye ulemavu.
‘’Bado jamii haitaki
kukubali kuwa, Watoto wenye ulemavu wana haki sawa kama binadamu wengine na badala
yake wanawekwa ndani na hawapewi haki zao za msingi ’’ Amesema Fakihat kwa
masikitiko.
Katika ulimwengu ambao
mara nyingi huhusisha mafanikio na ukamilifu wa kimwili na kiakili ni muhimu
kufahamu kuwa kuna watu wenye ulemavu ambao wamevuka changamoto.Hio na kutenda
mambo makubwa katika jamii ambayo yanaweza kuwa mfano wa kuigwa duniani. Fakihat
Omar Abubakar 23, ni Afisa Tehama katika Ofisi ya Jumuiya ya wanawake wenye
ulemavu Zanzibar – JUWAUZA. Amesema ‘’Watoto wenye ulemavu, bado hawapewi haki
yao ya elimu kama watoto wengine, wasio na ulemavu na vigumu kutimiza ndoto
zao’’Amesema Fakihat ambaye pia ni mwanaharakati wa masuala ya usawa kwa jamii.
Akiwa mtoto wa pili
wakike,kati ya watoto watatu wa familia ya Omar Abubakar, anayeishi Tomondo
Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja.Alizaliwa mwaka 2000 na alipata ulemavu akiwa mtoto, madaktari
walisema alichelewa kulia wakati anazaliwa ndio ikapelekea athari katika ubongo
wake na baadhi ya viungo.
Licha ya changamoto
hiyo, Fakihat haikumzuia kusoma na kutimiza ndoto zake za kielimu, amesema
alipata elimu yake ya maandalizi hadi kidato cha nne katika skuli ya Al falah
iliyopo Mombasa mjini Unguja.
Fakihat amesema,
elimu jumuishi kwa watu wenye ulemavu
haiko sawa kwa hapa Zanzibar, ambapo alishindwa kufaulu vizuri ,hii ni kwa sababu hakuweza kuandika
vizuri kutokana na mikono yake kutetemeka hivyo, walimu walishindwa kumzingatia wakati wa
usahihishaji wa mitihani kama mtu mwenye ulemavu.
Amesema, baada ya
matokea ya mitihani alishindwa kuendelea
na masomo ya elimu ya juu, na
kujiunga na chuo Cha Mamlaka ya
Elimu na Mafunzo ya Ufundi –VETA ili
kusomea ufundi wa maswala ya Tehama.Licha ya mapungufu yake ya kimwili yaliyosababishwa
na ugonjwa huo,Fakihat aliendelea kusoma kwa bidii na kuthibitisha kwamba,nguvu
za akili zinaweza kuvuka vikwazo vya kimwili.‘’Nilishawahi kupata mafunzo ya
uongozi kule Jambiani, na yananisaidia kutetea haki zetu za watu wenye
ulemavu’’Amesema.Fakihat.
Kilichomshawishi kupata mafunzo ya uongozi
ni kutokana na kuwa, na malengo ya kuwa kiongozi hapo baadae, ili awasaidie watu wenye ulemavu
kwani kuna pengo kubwa analiona.’’ Sisi watu wenye ulemavu bado kuna pengo ambalo lipo kwani bado hatuja shirikishwa vilivyo
katika kugombea nafasi za uongozi ‘’ Amesema Fakihat ambaye ana ndoto za kuwa kiongozi, lakini pia anatarajia kuingia
katika katika michakato wa kugombea nafasi mbali mbali za uongozi.
“Lengo langu hapo,
baadae ni kugombea nafasi za uongozi ili kuwatetea watu wenye ulemavu, katika
mambo yanayowahusu lakini pia kuwaletea maendeleo katika jamii kwa ujumla” amesema Fakihat.
Omar Abubakar ni baba
mzazi wa Fakihat, amesema licha ya kuwa na changamoto ya ulemavu ila amehakikisha anamsaidia binti yake kutimiza ndoto zake.‘’Kwa kweli najivunia
mwanangu, anajitoa sana kwa watu wenye ulemavu na kuitaka jamii, kujua haki za
watu wenye ulemavu na kuwasaidia kufikia ndoto za kielimu’’Amemaliza Omar.
Omar amesema kuwa, ni
vyema wazazi wawasaidie watoto wao, wote bila ya ubaguzi ili watimize ndoto zao za kielimu ili kuja kuwa
kiongozi wazuri baadae.‘’ Sisi wazazi tuna jukumu kubwa la kutimiza ndoto za watoto
wetu, hususani hawa wenye mapungufu ili kuwa viongozi wazuri ’’ Amesema Omar.
Mwana sheria kutoka
Jumuiya kwa ajili ya watu wenye ulemavu
wa akili Zanzibar ZAPDD Halfan Amour amesema, watu wenye ulemavu wana haki sawa
na binadamu wengine, ikiwemo haki ya kupatiwa elimu na kushiriki katika
kugombea nafasi za uongozi.“Watu wenye ulemavu wana haki zote,sawa na binadamu
wengine ikiwemo kupatiwa elimu na kushirikishwa katika kugombea nafasi za
uongozi ‘’Amesema Halfan.
Sheria ya watu wenye
Ulemavu, namba 6 ya mwaka 2006, imetamka wazi kuwa watu wenye ulemavu wana haki
zote za msingi kama binadamu wengine, ikiwemo kupatiwa elimu na haki ya kuwa
kiongozi.
Mtaalamu wa maswala ya
mawasiliano Jumuiya ya Wanawake wenye Ulemavu Zanzibar –JUWAUZA,Hawra Shamte
amesema lengo la kwanza la Fakihat
kuletwa ofisini hapo,ilikuwa ni kumuwezesha kujihudumia mwenyewe kwani
hapo awali, alikuwa anakaa ndani tu bila ya kutoka na kujishuhulisha na kazi za kijamii.‘’Lengo
kuu la Fakihat lilikuwa ni kuja hapa ofisini, kujichanganja na watu kwani, alikuwa
amesoma lakini wazazi wake walikuwa wanaendelea kumlea,hivyo mwenyekiti wa
JUWAUZA akaona aletwe hapa ofisini’’ Amesema
Bi Hawra huku akiongeza kuwa,
nafasi ya Fakihat kuja JUWAUZA, amekuwa mweledi kazini na anafanya kazi zake
vizuri , lakini pia na mtetezi wa haki
za watu wenye ulemavu Zanzibar.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake
Wenye ulemavu Zanzibar- JUWAUZA Salma Saadat, amesema kuwa
jamii ibadili mtazamo wao juu ya watu
wenye ulemavu na kuwapatia elimu
ili wasome na waje kuwa viongozi.’’Jamii
inapaswa ibadili mitazamo yao kuhusu watu wenye ulemavu na wawaone kama
binadamu wengine, na wawape haki zao zote za msingi ikiwemo elimu ili waje kuwa
viongozi wazuri baadae’’. Amesema Salma Saadat.
Post a Comment