TAMWA ZNZ, ZAFELA NA PEGAO KUADHIMISHA SIKU YA MTOTO WA KIKE OKTOBA 17
CHAMA cha
Wandishi wa Habari wanawake Tanzania Zanzibar, (TAMWA ZNZ) kwa kushirikiana na jumuia ya wanasheria
wanawake Zanzibar (ZAFELA) , jumuiya ya wanawake wenye ulemavu Zanzibar (
JUWAUZA) na Jumuiya ya Mazingira , Jinsia
na Utetezi Pemba, PEGAO, wataadhimisha
siku ya mtoto wa kike itakayo fanyika Alhamis, oktoba 17 ,2024, saa
mbili za asubuhi katika ukumbi wa ZURA Maisara
Unguja.
Katika
maadhimisho hayo, kutakuwa na uwasilishaji wa tathmini ndogo ya kuangalia ,
nafasi za uongozi kwa mtoto wa kike
katika ngazi za skuli za msingi, sekondari na vyuo vikuu, tathimini ambayo
itatoa mwanga wa kuweka kipaumbele kwa ajili ya kumuanda na kumnyanyua
mtoto wa kike katika kushika nafasi za uongozi.
Hafla
hiyo,itawashirikisha washiriki 70 wakiwemo, Watoto wenyewe, asasi za kiraia,
taasisi za kiserikali na walimu ambapo ujumbe wa mwaka huu ni ‘ MUWEZESHE MTOTO
WA KIKE, APAZE SAUTI YAKE’ wenye lengo la kuhimiza usawa wa kijinsia kwa kumpa
mtoto wa kike fursa sawa za uongozi katika ngazi za awali ili aweze
kufikia ndoto zake bila vikwazo
vyovyote.
Pamoja na
mikakati inayotekelezwa na wadau mbali
mbali, Watoto wakike bado wanakumbana na changamoto nyingi zikiwemo udhalilishaji , kutopewa
fursa sawa na Watoto wa kiume, na
mitazamo hasi ya kiutamaduni inaowanyima
haki za msingi zikiwemo nafasi za
uongozi.
Aidha, siku ya Mtoto wa kike Duniani
huadhimishwa oktoba 11 kila mwaka. Siku hii ilianzishwa na umoja wa mataifa
mwaka 2012 ili kuangazia haki za wasichana
na changamoto wanazokumbana nazo dunini kote, lengo lake ni kuhamasisha
juhudi za kuboresha fursa za elimu, Afya , Ulinzi na usawa wa kijinsia
kwa wasichana na kuhimiza wadau kuhakikisha wanatatua changamoto zinazomkwamisha mtoto wa kike kufikia ndoto
zake hasa katika uongozi.
MWISHO

Post a Comment