SOKA LINAVYOWEZA KUMNUFAISHA MTOTO WA KIKE


 

NA MARYAM NASSOR, ZANZIBAR

SOKA ndio mchezo maarufu zaidi duniani, hakika ni mchezo unaofuatiliwa zaidi kwenye sayari hii, kutokana na  mvuto wake wa kimataifa.

Wanasoka ndio watu wenye  umaarufu  mkubwa, kutokana na kuwa na majina makubwa.

 Ni Kweli, kwa hapa Zanzibar ukizungumzia soka la wanawake huwezi kuacha kulitaja jina la  Binasra.

Ni mkufunzi ambae anatambulika na shirikisho la mpira wa miguu la Afrika  (CAF)na lile la kimataifa (FIFA).

Pia  amesoma na kupata  leseni yenye gredi ‘A’ kwa Tanzania ni mwanamke pekee, na kwa  wachezaji wa Zanzibar ni hazina ambayo wanatakiwa  wachezaji wakike kuitumia.

Akizungumza na mwandishi wa makala haya, katibu wa chama cha mpira wa wanawake Zanzibar Neema Machano Othman, anasema mpira wa timu za wanawake umekuwa ukilinganisha na hapo awali.

Kwa  hapa Zanzibar, kuna walimu wazuri ambao wanajulikana kimataifa, hivyo ni rahisi kwa wachezaji  kujifunza na kufikia ndoto zao za kimichezo.

‘’ Hapa kwetu Zanzibar soka la wanawake, limekuwa ukilinganisha na hapo awali miaka mitano iliyopita tulianza na timu tatu tu ‘’alisema.

 Aidha alisema kuwa, Lakini kwa sasa wamefika  hadi timu kumi, ambazo unguja ziko nane na Pemba ziko mbili.

Saada Saidi mchezaji wa timu ya  wanawake ya warrious, alisema soka la Zanzibar linakuwa na wanamalengo  makubawa ya kimichezo lakini tatizo kubwa ni ufadhili katika ligi ya wanawake.

Alisema kuwa, ligi ya wanawake bado inasuwa suwa ukilinganisha na ligi ya wanaume, kutokana na kuwa bado soka la wanawake halijaaminika hapa Zanzibar , kama kule Tanzania bara.

“ Kule kwa wenzetu bara , ligi ya wanawake inapata wadhamini wa kuidhamini ligi na wachezaji wanafikia ndoto zao, kama oppa clement  ambae anachezea timu ya misri na mshahara wake ni mkubwa” alisema.

Aidha aliwataka wadhamini kujitokeza kuidhamini ligi ya wanawake hapa Zanzibar, kwani ligi imesimama kutokana na kukosekana kwa mdhamini.

Hafidha Juma Ali, ni mchezaji wa timu ya New Generation ya wanawake, anasema  michezo  ni afya pia nia ajira, lakini Serikali kama mdau nambari moja ije na mipango endelevu ya kuinua na kuihamisha ili iwe ajira kwa vijana.

Alisema kuwa, soka la wanawake bado linakabiliwa na changamoto lukuki hasa kwenye udhamini, hivyo serikali idhidi kuweka mazingira mazuri  na kuwatafutia mdhamini kutokana na kuwa wao ndio wanaanza hawajaaminika na wafadhili.

“ Tunahamu na sisi wachezaji kutoka Zanzibar tucheze timu kubwa za kulipwa , na ari na moyo wa kujituma tunao, lakini  bado soka la hapa kwetu linasua sua’’ alisema.

Juma Mohamed Juma kocha wa timu ya wanaume mwembeladu sc, anasema soka la wanawake linakuja vizuri kwa sasa kutokana na hapo awali lilikuwa halina hamasa.

Alisema kuwa, wachezaji wa kike wasikate tamaa kutokana na vikwazo vilivyopo na kupambana kuonesha uwezo wao, kwani’ hata mbuyu ulianza kama mchicha’.

 Hivyo, aliwataka wapambane kujituma kwani mpira wa wanawake na wanaume uko tofauti, na hata hapo zamani ligi ya wanaume ilikuwa haina mdhamini, lakini baada ya kupambana wamefanikiwa kuupata udhamini.

Nae katibu wa shirikisho la mpira wa miguu Zanzibar ( ZFF) Hassan Ahmada Vuai alipokuwa akizungumza na mwandishi wa makala haya alikiri kuwa ligi ya soka la wanawake imesimama kutokana na kuwa haina udhamini.

Alisema kuwa,  bado hawajapata wadhamini wakuiidhamini ligi ya wanawake, hivyo wanaziomba taasisi binafsi kujitokeza kuidhamini ligi hiyo.

Aidha alisema kuwa,  ligi ya wanawake imekosa sapoti kutokana na kuwa jamii bado hawajataka kubadili mitazamo yao, na kuona mwanamke popote anaposhiriki basi anafanikiwa mfano mzuri niRaisi wa jamuhuri wa Tanzania anavyosonga  mbele.

Hija Mohamed Ramadhani, mshauri wa maswala ya jinsia katika michezo kutoka shirika la Ujerumani (G IZ)hivi karibuni alipokutana na wandishi wa habari, alisema mradi wa michezo kwa maendeleo hapa Zanzibar  utaboresha mazingira mazuri ya mindombinu ya viwanja na inalengo la kujenga viwanja saba Unguja vinne na Pemba vitatu .

Lakini ipo haja kwa shirika hilo na taasisi nyengine kujitoa zaidi kudhamini ligi za timu za wanawake ili kuwapa hamasa na kuiona hasa ile dhana ya michezo kwa maendeleo inavyofanya kazi kwani waswahili wanasema ‘ kuona  ndio kuaminii’.

     MWISHO

 

 

No comments

Powered by Blogger.