WANDISHI WA HABARI KUHAMASISHA USAWA WA KIJINSIA MICHEZONI





NA MARYAM NASSOR

 WAANDISHI wa habari nchini wametakiwa kuhamasisha wauguzi wa kike kuingia katika kada ya uguuzi na tiba michezoni ili iwe hamasa kwa watoto wa kike kushiriki katika soka.

 Akizungumza katika mafunzo ya siku tano ya wandishi wa habari za michezo huko
 ofisi ya TAMWA ZNZ, Tunguu Unguja, mwandishi na mhariri wa habari za michezo kutoka gazeti la Zanzibar leo, Salum Vuai.

 Alisema, kumekuwa na uchache wa wauguzi wa kike katika michezo, au katika timu nyengine hakuna kabisa kwa hapa Zanzibar.

 “ Kama munataka wanawake wengi kushirikia katika michezo, basi ni vizuri kwanza muwahamasishe wauguzi wakike kuingia katika tasnia ya michezo ili wawastiri wenzao wanapopatwa na shida viwanjani’’ alisemAa






 Aidha aliishauri Serikali kurejesha ruzuku katika vyama vya michezo ili isaidie kuajiri wauguzi hao, kutokana na kuwa timu nyingi za wanawake ni maskini hivyo ni vigumu kutekeleza hayo.

 Nae, mkufunzi katika mafuzo hayo Bi hawra Shamte aliiwataka wandishi wa habari kuhamasisha wanawake kushiriki katika michezo kwa maendeleo kutokana na kuwa michezo ni ajira .

" Siku hizi mpira ni ajira , tumekuwa tukisika timu za kiume wachezaji wananunuliwa kwa bei ghali hivyo, wanaweza kujiajiri kupitia michezo kwa kutumia dhana ya michezo kwa maendeleo,"alisema.






 Alisema kuwa, licha ya kuwepo katiba na sera ya michezo ya mwaka 2018 lakini bado kuna ushirikishwaji mdogo wa usawa wa kijinsia katika michezo. Hivyo, aliwataka wandishi wa habari kuihamasisha jamii katika ngazi ya familia, ili wazazi waruhusu na kusaidia wasichana kushiriki katika michezo

. Nao, baadhi ya washiriki katika mafunzo hayo, waliahidi kufanya kazi kwa bidii ya kuihamasisha jamii ili kuruhusu wasishana na wanawake kushiriki katika michezo kama haki yao ya msingi ya kikatiba.

 Programu ya michezo kwa maendeleo, inatekelezwa na TAMWA ZNZ, ZAFELA na Cente for Youth Dialogue kwa kushirikiana na Deuth Gesellschaft fur intetnational Zusammenrbeit (GIZ) shirika la Ujerumani ikiwa na lengo la kuhamasisha waandishi wa habari kuandika bahari za michezo na ushirikia wa wanawake katika michezo.
          
                                       MWISHO

No comments

Powered by Blogger.