WAANDISHI WA HABARI ENDELEENI KUPAZA SAUTI ZA WANAWAKE -TAMWA ZNZ

NA MARYAM NASSOR 


WAANDISHI wa Habari wametakiwa  kuendelea kuandika Habari za wanawake ambao bado sauti zao hazijasikika  katika kukabiliana  na  mabadiliko ya tabianchi .

 Akizungumza   na wandishi wa Habari , Meneja miradi kutoka Chama cha   wandishi wa Habari wanawake   Tanzania Zanzibar( TAMWA ZNZ)   Nairat  Abdulla   huko katika Afisi za chama hicho Tunguu.

Amesema,  wanawake wengi wanafanya kazi kubwa katika  kukabiliana na mabadiliko  ya tabianchi kwa kulima  na kuhifadhi mikoko lakini jitihada zao hizo bado hazijaonekana katika jamii. 

Amesema kuwa, utafiti uliyofanya na chama hicho umebaini kuwa  bado uwepo na ushiriki wao katika shughuli hizo haujapewa kipaumbele ipasavyo, kupitia vyombo vya habari .

“ Utafiti tuliyofanya TAMWA, ZNZ  umegundua  bado sauti  za wanawake  hazijasikia ipasavyo kupitia vyombo vya Habari katika  kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi , hivyo  wandishi wanapaswa kuongeza  nguvu katika eneo hilo” amesema Nairat.

 Nae,  Meneja Mashiriano ya Kimataifa kutoka  Jumuiya ya Kutunza Mazingira ya Kimataifa  ( CFI ) Lilian Simule amesema,  mradi wa Zanz Adapt  wanahamasisha wakulima viongozi  kutumia vyombo vya Habari kutangaza kazi zao.

Amesema kuwa, mradi huo unawawezesha wakulima kulima  kilimo mseto na   kilimo biashara, hivyo ni vyema kujitangaza ili jamii ijuwe wanafanya nini katika kutunza mazingira na  kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Aidha kwa upande wake, Meneja wa Mawasiliano  kutoka TAMWA,ZNZ  Sophia Ngalapi alisema  waliona kuna umuhimu mkubwa wa  kurejea mafunzo hayo kwa wandishi wa Habari ili kuwaweka sawa.

“ Tumeona ipo haja kubwa kuyarejea haya mafunzo ili kusikiliza maoni yenu na kukumbushana maeneo ya mradi huu ili musiende kinyume” alisema Ngalapi. 

 Nae, Afisa Kilimo Msitu Rhoda  Daniel Kadaso  alisema mradi huo  umeanzisha vitalu vya miche ya misitu na mboga mboga   kwa  lengo la kuwasaidia  wakulima wa mradi huo,  kupata  miche bora na kwa wakati ili kuongeza kipato chao.

  tuliwatowa wakulima wa mazao  kutoka hapa Zanzibar  Kwenda Tanzania bara ili kupata   uzoefu na kujifunza  kilimo zaidi na  kuona jinsi gani wenzao wanalima na kupata faida”

   Nae, Afisa Mawasiliano kutoka Jumuiya ya  kuhifadhi Misitu Pemba ( CFP) Munira Kaoneka amesema  katika mradi huo wanataka wandishi  wa  habari kuandika zaidi katika  kuwahamasisha  wanawake   kuona umuhimu wa  kumiliki ardhi .

Amesema  kuwa, wanawake wengi hawamiliki ardhi hasa huko vijijini ,na  wanaomiliki  hawana hati za umiliki wa ardhi kisheria .

  Tunataka wandishi wahamasishe wanawake waone umuhimu wa kumiliki ardhi lakini pia wawe na hati za umiliki kisheria ili ” amesema Munira.   

   Mafunzo hayo, ya siku tatu  yameandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari Tanzania Zanzibar( TAMWA ZNZ,)  Jumuiya ya Kuhifadhi Misitu Pemba ( CFP)  na Jumuiya ya Kuhifadhi Mazingira Kimataifa ( CFI)  na kuwashirikisha wandishi 20 waliyokuwemo katika mradi huo.


                                  Mwisho


No comments

Powered by Blogger.